Unyanyasaji ni nini?

Naomba mtu mwenye tafsiri sahihi ya unyanyasaji
Ni jumla ya matendo yote yanayoweza kumuathiri Mtoto Kimwili, Kiakili, Kihisia na Kijamii. Mfano Kumpiga, Kumnyima chakula, Kumchoma moto mikono n.k
- 1 amependezwa
kumtenda mtu kinyume na anavyostahili
Ni kumtendea mtu mwingine matendo yanayomsababishia maumivu kimwili au kihisia.
Ni vitendo na mitazamo yote ya udhalilishaji na uporaji wa haki na utu wa mtu
Ni ukatili wa aina yote na kuondoa haki ya mtu